KHADIJA MKE WA MTUME 3


Haukupita muda mrefu bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akaolewa na Nibash bin Zirarah Al Tamimi aliyekuja kujulikana kwa jina la ‘Abu Halah”,  na wakapata watoto wawili waliowapa majina ya Hind na Halah.

Waliishi kwa wema mpaka mumewe wa pili naye pia alipofariki dunia, na haukupita muda mrefu baba yake Bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) naye pia akafariki dunia, jambo lililozidisha huzuni moyoni mwake. (zipo riwaya zinazosema kuwa baba yake bi Khadija alifariki dunia baada ya binti yake kuolewa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Laahu alayhi wa sallam) na kwamba yeye ndiye aliyeifunga ndoa yao. Hata hivyo riwaya zenye nguvu zaidi zinasema kuwa alifariki kabla ya bibi Khadija kuolewa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Laahu alayhi wa sallam) na kwamba aliyefunga ndoa ya bibi Khadija na Mtume (Swalla Laahu alayhi wa sallam)alikuwa kaka yake anayeitwa Amru bin Khuwaylid.

Baada ya misiba hiyo iliyofuatiliana, Bibi Khadija aliyerithi mali nyingi sana kutoka kwa baba yake na kutoka kwa waume zake waliofariki, aliamua kujitenga na watu akawa anajishughulisha na ulezi wa wanawe.


Watu wengi walipeleka posa kutaka kumuoa, lakini Bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) aliwakataa kwa sababu alihisi kuwa wote hao walikuwa wakimtaka kwa ajili ya tamaa ya mali yake na uzuri wake.

No comments

Powered by Blogger.