KHADIJA MKE WA MTUME 1
Nasaba yake
Jina lake ni Khadija binti Khuwaylid bin Asad bin Abdul Uzza Qusay bin Kilab anayetokana na kabila la Kikureshi aliyezaliwa katika mwaka wa 68 kabla ya Hijra yaani mwaka 556 baada ya Nabii Issa (Alayhis Salaam).
Wazee wake walimlea kwa heshima na adabu ya hali ya juu na alikuwa akijulikana kwa jina la ‘Aliyetakasika’ hata kabla ya kuja kwa Uislamu.
No comments